Moja
ya habari iliyoripotiwa ni hii kutoka gazeti la Mwananchi, yenye kichwa
cha habari ‘simu bandia zapata soko Msumbiji, Congo’.
Gazeti
hilo limeripoti kuwa Siku mbili baada ya mamlaka ya mawasiliano Tanzania
(TCRA) kuzima simu feki, wafanyabiashara wa simu hizo wamepata soko
jipya katika nchi za Msumbiji na Congo.
Wakizungumza kwa nyakati
tofauti na gazeti hilo, baadhi ya vijana waliokutwa wakizunguka madukani
kuzikusanya, walisema wanazinunua na kuzisafirisha kwenda huko kwa
ajili ya kuziuza kwa watumiaji. Walisema katika nchi hizo kuna soko kwa
sababu zinakamata mawasiliano kama kawaida.
Gazeti hilo
limemnukuu Lawrence Kyondo ambapo amesema wanazinunua kwa bei ya
makubaliano na kwenda kuziuza katika soko la
nje……….>>>’hatujaanza hii biashara leo, siku nyingi isipokuwa
wenye maduka walikuwa bado wagumu kuziuza wakidhani hazitazimwa’
-
Blogger Comment
-
Facebook Comment
Subscribe to:
Post Comments
(
Atom
)
0 comments :
Post a Comment